Na: Erwin Kinsey, Mkurugenzi wa ECHO – Kanda ya Afrika Mashariki
Limechapishwa: 26-02-2014


Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 1Yaliyomo katika mada hii ni mapendekezo ya ECHO kuhusu njia bora tunazozikuza kuwasaidia  wafugaji. Katika kuandaa makala haya  Mkurugenzi wa ECHO kanda ya  Afrika Mashariki ndugu, Erwin Kinsey, ametumia uzoefu wake wa shughuli za maendeleo ya jamii na utaalamu wa kilimo na ufugaji wa miaka mingi aliyoishi nchini Tanzania. Katika machapisho mbalimbali ya ECHO, yaliyotumika katika kuandaa makala haya ni pamoja na;  ECHO Development Notes ( EDN ),Technical Notes (TN), na ECHO East Africa Symposium (EEAS) presentations. Nyingi ya nyenzo hizo pia zilikusanywa kutoka kwa wataalam na vikundi vingine ambavyo kumbukumbu na machapisho zimeorodheshwa. Katika makala haya picha  zimetolewa kwa hisani ya ndugu Erwin Kinsey. 

Utangulizi

Ufugaji mifugo kiasili unaelezewa

Ufugaji wa mifugo kiasili ni mfumo wa maisha ambao watu au jamii husika wanaishi maisha yao kwa kutegemea mifugo. Katika ukanda wa Afrika ya Mashariki, wafugaji hawa hutegemea zaidi mifugo ya aiana mbali mbali kama; ng’ombe, kondoo, mbuzi, punda, na ngamia ili kukimu maisha yao na familia zao. Mifugo iliyotajwa, imeorodheshwa kwa kigezo cha kuanzia na lile kundi ambalo sio stahimilivu sana (ng’ombe) na kumalizia na lililo stahimilivu zaidi (punda na ngamia), pia kwa kuzingatia maeneo ya ufugaji kuanzia na yaliyo makame kiasi hadi makame zaidi.

Wafugaji hawa wana mchango mkubwa sana katika sekta/idara husika lakini bado hawajaweza kuthaminiwa ipasavyo. Kwa mfano: uwezo wa kutunza/kuendeleza kizazi cha ng’ombe wa asili. Katika utunzaji wa mifugo yao, wafugaji hawa wana uwezo wa kipekee wa kutumia maeneo yanayokabiliwa na ukame kwa njia ya kuhama hama kwa ajili ya kupata malisho bora na maji. Ni ukweli usiopingika kwamba, katika/ ukanda wa Afrika ya mashariki maeneo ya hifadhi nyingi tunazozifurahia kwa sasa ni matokeo ya wafugaji kuhamahama na kuweza kuyatunza maeneo haya kwa ajili ya malisho na hasa kuweza kuyalinda/kuzuia yasiingiliwe na shughuli za kilimo.

Transhumant pastoralists usually migrate between two or more permanent settlements, alternating between the same locations; they rely less upon animal products alone, often engaging in seasonal farming, and are more likely than nomads to be engaged in marketing their produce (O’Neil 2011). Most pastoralists are nomadic, transhumant, or some variation of the two.

Ili kupata uelewa sahihi wa ufugaji wa kiasili yaani ufugaji wa kuhamahama, ni vyema kujua maana halisi ya maneno muhimu yanayowakilisha mfumo huu ambayo ni; 

Nomadisim: hali ya kutokuwa na makao/makazi ya kudumu. Hapa xwafugaji hubeba vitu vinavyohamishika na kuhamahama pamoja na mifugo yao katika kutafuta malisho bora na maji. Mfumo huu hubadilika kulingana na misimu ya hali ya hewa kwa mwaka husika. Sehemu kubwa ya chakula kwa wafugaji wa aina hii, hutegemea kutoka kwenye mifugo yao yaani (nyama na maziwa) na vile vya kukusanya msituni/porini ( matunda, asali n.k)  

Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 2Vijana wa kiume hujipatia umaarufu kwa kufanya vitendo vya kijasiri kama vile kufukuza wanyama wakali hasa wale wanaoweza kudhuru mifugo kama vile simba. Baadae katika maisha yao ya baadae, hii itawawezesha kujipatia mifugo mingi, wake wengi na hatimae watoto wengi.

Wanawake wanao wajibu wa kutunza watoto, kujenga nyumba, kukusanya kuni, kutafuta chakula na kupika.

A strong emotional attachment to livestock. Beyond being a primary means of asset accumulation, pastoralists also use animals for draught power, rituals, food and trade.

Swala la kijinsia katika jamii hii ni la kipekee sana na halitambuliki kirahisi. Hata hivyo lina faida na hasara zake (Hodgson2011)

Wanawake hawana sauti katika maswala ya kisiasa.Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 3

Wanawake wametengwa katika mambo mengi yanayohusu maisha ya kila siku.

Hata hivyo, wanawake wana nguvu sana katika usimamizi wa baadhi ya vitu kama maziwa, mifugo midogomidogo (kuku,mbuzi na kondoo) na wanaweza kuendeleza maisha yao wenyewe  kutokana na kipato wanacho kipata.

 

Changamoto

Wafugaji wa kiasili ni kati ya watu wasio na uhakika wa chakula duniani. Maisha/uhai wao hutegemea haswa mifugo kwa kiwango ambacho mifugo imekuwa ikipewa kipaumbele katika kufanya maamuzi hata katika mambo yanayohusu mwanadamu/ubinadamu.

Mifugo yao iko hatarini mara kwa mara kutokana na ukame na magonjwa, na pia wakati mvua na ukame vikiwa havitabiriki katika nyanda kame kiasi na kame zaidi. Hali imewahi kuwa mbaya zaidi katika kumbukumbu za Afrika katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Matokeo ya ukame huo ni mabaya kabisa katika maeneo ya wafugaji licha ya ubunifu wao wa kukabiliana na majanga kama haya. (Catleylt et al. 2002).

  • Milipuko ya magonjwa pia imekuwa katika kiwango cha hali ya juu katika maeneo mengi.
  •  Kupotea kwa ndama wengi zaidi ya asilimia 50 katika miaka ya kawaida kutokana na magonjwa yanayozuilika mfano ndigana kali.
  • Mlipuko wa magonjwa yasiokuwa ya kawaida hasa wakati wa mvua mfano homa ya mapafu [CBPP],homa ya mbuzi ya midomo [PPR], ulimi wa blue [blue tongue] n.k.

Wafugaji hawa wamekuwa wakipata hasara kwa karne nyingi hata kabla ya ukoloni.  Katika maeneo mengi duniani, imekuwa ikiwapasa kumudu mazingira magumu na mabadiliko ya kihistoria yaliyotokea tangu karne ya 19 hadi leo. Mabadiliko haya yanajumuisha yafuatayo;

  • Ongezeko la watu
  • Kupungua kwa ardhi ya malisho; aidha kutokana na kilimo au kuhamishwa na serikali
  • Kupungua kwa mifugo kutokana na magonjwa ya kigeni kama kulipotokea ugonjwa wa sotoka (rinderpest)
  • Kushindwa kwa tawala zilizokuwepo na kutokupata huduma muhimu wakati na baada ya ukoloni kutokana na zama hizi kutokuelewa dhana nzima ya matumizi ya aridhi na rasilimali nyinginezo kwa mfumo uliokuwepo wa ufugaji wa kiasili
  • Umasikini/kufilisika kutokana na ukame wa mara kwa mara na kumomonyoka kwa maadili ya  dhana shirikishi ndani ya jamii.

Baadhi ya serekali za mataifa machache zimeweza kukubaliana vyema na soko la mifugo ya wafugaji wa kiasili kuwa katika mfumo wa rasmi. Hata hivyo, ipo changamoto ambayo ni, kushindwa kuthamini/kutambua ufugaji huu wa kiasili kwamba unao umuhimu wa kiuhifadhi wa mifugo inayokuza uchumi japo katika mfumo usio rasmi au uwezo wao wa kutumia nyanda kame ipasavyo kuliko wazalishaji wengine. Vilevile, baadhi ya tawala/serikali zimekuwa zikifanya jitihada za kuwazuia wafugaji hawa wasihamehame na wawe na makazi ya kudumu kama kigezo cha kuweza kuwapatia fursa sawa za huduma za kiafya, kielimu na miundo mbinu nyingine kama barabara.

Wafugaji hawa wamekuwa wakilazimika wapunguze idadi ya mifugo yao kama njia ya kuzuia uharibifu wa ardhi ikiwa ni pamoja na kutozwa kodi kulingana na idadi ya mifugo uliyo nayo jambo ambalo limekua gumu kwao kuridhia.

Sera za aina hii zimekuwa zikiwanyima fursa wafugaji mmbadala wa kutumia mikakati hai mbalimbali waliyo nayo kulingana na elimu yao ya kiasili ili waweze wenyewe kuoanisha idadi ya mifugo waliyo nayo na malisho yaliyopo (EI Hadary 2012; Scoons 1995)

Changamoto nyingine nyingi zimechangia wafugaji kuathirika kupitia mambo ya asili na yale yanayosababishwa na mwanadamu ijapokuwa, changamoto hizi madhara yake yanatofautiana au kuingiliana. Katika eneo hili changamoto hizi zimegawanyika katika makundi matatu tofauti nayo ni;

i. Changamoto za kihuduma-kisiasa-kitamaduni:

  • Migogoro kati ya wafugaji na wakulima na serikali kuhusu ardhi na vyanzo vya maji ambavyo huchangia wafugaji kuwekwa pembezoni katika kupatiwa huduma  bora  za kijamii kama elimu na afya na hata kutoshirikishwa ipasavyo katika nyanja za kisiasa. 
  • Usalama duni unaohusisha wizi wa mifugo hasa maeneo ya mipakani kwa kuvamiwa mara kwa mara.
  • Ugumu wa kuanzisha mtandao wa kiusalama kutokana na uchache wao kulinganisha na ukubwa wa maeneo wanamoishi. Hii inatokana na ukweli kwamba wafugaji wanaishi kwa kutawanyika ambapo kuhamahama kwao ni kwa msimu na kunahitaji kaya  kugawanyika 
  • Uhaba au uchache wa aina tofautitofauti za vyakula katika milo ya kila siku ikiwa ni pamoja na vile vyakula vyenye lishe bora zaidi.
  • Kiwango kidogo/cha chini cha virusi vinavyosababisha magonjwa ya ukimwi (HIV/AIDS) kwa wanaume waliotahiriwa kinawaweka katika hali ya hatari zaidi ya kujamiiana kufanya wanawake kuwa katika hatari zaidi ya kuambukizwa ugonjwa wa UKIMWI.

Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 4

ii. Changamoto za kimazingira 

  • Wingi wa mifugo: 
    • Kukosekana kwa malisho bora
    • Kukosekana kwa mipango mizuri/endelevu ya kulisha mifugo
    • Matumizi ya kupita kiasi ya maeneo yanakopatikana maji
    • Uharibifu wa /matumizi mabaya ya mali ya asili (ukataji miti, mmomonyoko wa ardhi, uchafuzi wa mito na chemchemu za maji, kupungua kwa uwezo wa maji kupenya ardhini na hatimae kushuka kwa kiwango cha maji ya asili)
  • Kupungua kwa mifugo kupita kiwango stahiki cha ufugaji wa kawaida
  • Mvua zisizokuwa za uhakika zinazopelekea ulazima wa kuhamisha mifugo kwenda kutafuta malisho yaliyo bora sehemu nyingine.
  • Kuingiliana katika malisho na wanyama pori kunakopelekea wakati mwingine kuambukizana magonjwa mfano kichaa cha mbwa, ugonjwa wa miguu na midomo, n.k
  • Hali ya hewa isiyo rafiki; joto kali nyanda za chini na baridi nyanda za juu ambazo kwa pamoja huathiri uhai wa binadamu, wanyama na mimea. 
  • Umbali; wanamoishi wachungi hawa ni mbali na huduma muhimu za kujikimu kimaisha ambapo inawalazamu kusafiri umbali mrefu kupata maji, mazao ya kilimo na bidhaa nyinginezo muhimu kwa matumizi ya nyumbani.

iii. Changamoto za kiuchumi: 

Umasikini  mkubwa na hali ya kutokua na uhakika wa chakula katika sehemu kubwa  ya jamii hii,  inatokana na changamoto zilizoainaishwa hapo juu pamoja na;

  • kushuka kwa pato la mwaka kutokana na kiwango kidogo cha uzalishaji ukilinganisha na ongezeko la watu na rasilimali chache zilizopo
  • Utajiri umelundikana kwenye kaya chache na kuwafanya wengine kufanya kazi kama vibarua na hivyo kubakia kama maskini katika jamii.
  • Matajiri wachache na wenye elimu, huwapatia wanajamii wengine; ajira zisizo rasmi, mikopo na kuwaandalia sherehe (vyakula na vinywaji). Matokeo yake ni udhaifu na kutokuwa mtandao wa kijamii unaoweza  kuwaondolea  umaskini 
  • Mgongano wa kimaslahi kati ya wanaume wanao miliki mhimili huu wa uchumi na wanawake walioachiwa shughuli za kuangalia mahitaji ya kaya.

Kwa taarifa zaidi kuhusu changamoto na umuhimu wa kulinda uhai/maslahi ya wafugaji angalia andiko la World Initiative for Sustainable Pastoralism.

Kanuni muhimu

Ni jinsi gani jamii za kifugaji zitavyoweza kumudu kukudhi mahitaji ya chakula katika mazingira yao wanayoishi? Katika sehemu hii inayofuata, tutaangalia kanuni muhimu za kuzingatia kama muongozo wa kufanya maamuzi wakati wa kuandaa unachotaka kufanya ndani ya jamii ya kifugaji kwa maendeleo yao. 

Hakuna majibu rahisi au mchakato wenye sura ya kipekee ambao unaweza kutumika katika kila hali inayojitokeza

Tabia nchi inatofautiana kutokana na maeneo ya nch, na pia kutokana na vitu vingine kama; sera, aina ya serekali na masoko. Vitu vyote hivi ni lazima vipewe kipaumbele na kuchanganuliwa katika kila mchakato wa kuwasaidia wafugaji. Kilimo cha mazao ya shambani chaweza kuwa mojawapo ya mpango mkakati mzuri wa kuwasaidia wafugaji wale wanaohamahama lakini kila waendako wana makazi maalumu (transhumant) tofauti na wale wasiokuwa na makazi maalumu (nomadic). Njia yeyote mmbadala ya kuwasaidia wafugaji hawa katika maisha yao tofauti na mifugo, ni lazima iendane na mazingira ya wafugaji ikiwa ni pamoja na kuruhusu ufugaji wa kichungi na utunzaji malisho na ardhi kwa muda mrefu katika kuzalisha. Angalia katika mtandao wa ECHOcommunity.org (ECHO Best Practices Note no.1 na soma kuhusu ECHO Best Practices Note no.1 soma kuhusu ‘improving degraded lands’).

Mabadiliko hayapukiki

Yamkini ya mabadiliko ya tabia nchi na yenye madhara makubwa, yanawaathiri wafugaji wa asili katika nyanja za ardhi/mazingira na hivyo; kuathiri upatikanaji wa rasilimali,kutokua na mbadala wa kujikimu au kuendesha mfumo wa maisha yao ya jadi, na kukosa fursa ya kuuza mazo yao. Katika maeneo mengine mabadiliko hutokea ambapo hutoa fursa za masoko na kuboresha maisha. Lakini kwa maeneo mengine, fursa zaweza kupotea kabisa na umaskini kukithiri. Lengo la wadau wa mabadiliko linatakiwa kuwa: kuongeza uwezo wa wafugaji kupambana na hali zinazowakumba na kuboresha maisha yao kwa ujumla.

Ufugaji pimifu (livestock ranging) ni njia muafaka ya kuendesha maisha ya wafugaji

Ufugaji pimilifu (livestock ranging) katika maeneo makame na yenye mvua chache ni mfumo wa maisha unaowezekana na unayokubalika katika maeneo ya wafugaji. Ustahimilivu wao kwenye ukame na matukio yasiyotabirika inadhihirisha ukweli wa mipango yao mikakati ya utunzaji wa mifugo inayojikita katika kuhamahama. Juhudi za maendeleo zinatakiwa kujumuisha sekta/idara ya huduma za mifugo na na kuanzisha njia mbadala na madhubuti ambazo zinategemewa kuzalisha yafuatayo:

  1. Kutoa manufaa kwa jamii yote kwa ujumla bila ubaguzi wa kundi lolote kati jamii na hasa kuhakikisha kutokua na tofauti kubwa ya kipato kati ya wanajamii.
  2. Matumizi yenye uwiano sawa wa rasilimali zilizopo

Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 4Mbinu shirikishi zitatoa hamasa ya umiliki

Ushirikishwai wa wafugaji katika kuchagua teknolojia muhimu zinazowahusu na hasa kwa kuzingatia jinsia na marika kama vipaombele vyao vilivyo tofauti tofauti. Tafiti nyingi zimeshafanyika katika nyanja ya kilimo na chache zimefanywa katika ufugaji hasa katika maeneo makame yenye mvua chache (semi arid). 

Kunahitajika utafiti zaidi

Hata hivyo ingekua ni vizuri tafiti nyingine zilizoonesha mafanikio katika nchi/maeneo mengine yanayofanana na haya kutiliwa maanani na nyingine nzuri kuigwa. Vilevile tafiti bado zinatakiwa kwenye maeneo haya. Hii itasaidia kuweka mikakati endelevu na kutumia teknolojia sahihi zilizojaribiwa kwenye jamii ziishizo maeneo kame katika shughuli za uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo.

Mbinu

Hakuna mbinu moja pekee inayotumika kila sehemu, lakini zifuatazo ni baadhi ya njia bora za ufanisi katika sehemu za wafugaji wa asili, juu ya matumizi ya ardhi, kuboresha mifugo, teknolojia za asili na usimamizi wa rasilimali. Angalia “Kwa Maelezo Zaidi” ukipata taarifa zaidi kuhusu mazoea.

Kuboresha maeneo ya malisho katika maeneo ya wafugaji

Njia bora na shirikishi za kuendeleza mipango ya matumizi ya ardhi,  maji na mazingira katika katika maeneo ya wafugaji ni pamoja na zifuatazo:

Mbinu: Kutumia njia shirikishi ili kusaidia jumuiya kuendeleza mipango ya matumizi ya ardhi (Maji - Bayer na Bayer 1994). Kuhakikisha wafugaji waanzishe sheria ndogondogo endelevu ili kulinda rasilimali kwa manufaa ya umma. Ikiwezekana, matumizi ya teknolojia [digital] ili kutengeneza ramani huongeza usahihi katika mipango ya matumizi ya ardhi.

Tree stumps pruned as per the FMNR method

Tree stumps pruned as per the FMNR method. Photo by Tony Rinaudo

Mbinu: Matumizi ya mifumo sahihi ya maliasili, kama vile:

  • Kuboresha uoto wa asili [FMNR], ni njia ya kulinda na kulea miti na kuruhusu kuchipua mashina ya miti ya asili yaliyokatwa. Njia hii ina mafanikio zaidi kuliko kupanda miti ya jadi.
  • Mkulima kutumia kilimo cha mseto [FMAFS]: Kupanda mchanganyiko wa miti na mazao ya asili na ya kigeni ili kuboresha mahitaji mbalimbali ya jamii.
  • Utunzaji wa mazingira wa jumla wa rasilimali (HM): Allan Savory ameanzisha vikundi vya HM katika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Vikundi vinadhibiti ufugaji holela kwa kuzingatia malisho ya mzunguko na maeneo yasirudiwe kulishwa hadi majani yanapochipua upya, hivyo kurejesha kwa kiwango kikubwa majani ya asili katika maeneo ya malisho. 

Mbinu/njia za kuboresha utunzaji wa mifugo katika maeneo ya wafugaji 

Mbinu: Kuwezesha upatikanaji/ utoaji wa chanjo wakati wa majanga mfano msimu wa mafuriko na/au wakati kuna uwezekano wa milipuko ya magonjwa. (Baadhi ya magonjwa yametajwa hapa chini)

Kuwahusisha wahudumu wa mifugo wa jamii waweze kuelezea/kutoa taarifa za visababishi na vienezi vya magonjwa yanayoathiri afya ya mifugo. Magonjwa yanayotakiwa kutambulika ni kama homa ya mapafu (CBPP), homa ya bonde la ufa (RVF), homa ya mbuzi ya midomo (PPR), ndigana kali (ECF) na kideri (ND).

Mbinu: Kusaidia kutambua na kudhibiti wadudu waenezao magonjwa (parasites). Hapa ni kujaribu kufikiria kuwawezesha wafugaji kwa njia ya elimu katika maeneo yao kuwafundisha wafugaji waweze kuwa na elimu kuhusu wadudu wanaoeneza magonjwa ya mifugo yao. Kutambua utegemezi wa dawa za asili katika kutibu mifugo –kwa mfano, dawa za asili za kupambana na wadudu wanaoeneza magonjwa ya mifugo, na ufugaji wa mifugo mbadala kama njia ya kupambana na magonjwa,pia kutambua ukweli kwamba mbuzi na kondoo kutoka jamii ya kifugaji walishajijengea hali fulani ya kinga kutokana na wafugaji kuwa na ujuzi wa jinsi wanavyochagua mifugo yao.

Mbinu:

  • Kuuweka utaratibu wakufidia mifugo inayopotea kabla au kwa haraka pindi yanapotokea majanga ya kiasili kwa kuzingatia mipango mikakati kama kununua mifugo ili wafugaji waweze kuwa na pesa taslimu kwa wale wenye mifugo mingi. Kwa wale wenye mifugo michache msaada wa chakula unaweza kuwa mbadala kuliko kununua mifugo yao.
  • Kurejesha mifugo ili kusaidia unafuu baada ya majanga ya ukame au magonjwa ya mlipuko iliyopunguza mifugo yao. Kuwa makini na vitu ambavyo vyaweza kufanywa ili kufaulu au kushindwaa kutokana n jitihada za kurejesha mifugo (Heffeman et al.2001). Jitihada hii ni muhimu sana kwa mafanikio hasa kwa wale wafugaji ambao ndio kwanza wamepoteza mifugo yao ukilinganisha na wale wazoefu wa kuhamaha. 
  • Kuhamasisha umiliki binafsi wa mifugo kama ilivyokuwa katika jadi zao na wahusishe kaya  kuchagua aina ya mifugo kwa kiwango ambacho wanakimudu katika utunzaji

Mbinu: Kundi la mifugo liwe sawia na mazingira wanamoishi/ maeneo ya malisho (Mace; 1988) hii itasaidia kupata uzalishaji bora na wa kiwango kitakachokidhi mahitaji ya kaya kwa kuwapatia nyama, na mazao ya maziwa. Utafiti wa UNHCR (1998) unaonesha kwamba ngamia wanastahimili mazingira magumu ukilinganisha na wanyama wengine kama mbuzi na ng’ombe. Hata hivyo wakichanganywa kutakua na uwiano bora kwani mbuzi na ngamia hula majani ya juu ili hali ng’ombe na kondoo hula majani ya chini.

Mbinu: Boresha koo za mifugo ya asili kwa kutumia au kuchanganya na koo bora zaidi itakayowezesha kutoa kizazi chotara ambao ni wastahimilivu na mazao yao ni maradufu zaidi kuliko koo za asili (kukua kwao ni kwa haraka, nyama nyingi na maziwa mengi) Mfano Borani/Sahiwal wakipandiana  na East African short horn zebu.

Uvunaji wa maji na matumizi yake kitaalam

Wafugaji wanaishi kwenye ardhi kame ambayo kwa kawaida ina uhaba wa maji hivyo kupelekea uzalishaji duni wa mazao ya kilimo na mifugo. Zifuatazo ni mbinu ambazo zitasaidia ongezeko la maji katika maeneo haya:

Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 5Mbinu:  Tengeneza maeneo ya kuhifadhia maji ya mvua kwa ajili ya matumizi ya kilimo na mifugo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha uwepo wa maji salama ya kunywa.

Vihifadhio vya maji ambavyo ni muafaka kwa jamii hizi ni hivi vifuatavyo;

  • Madibwi ya kujitengeneza kwenye udongo.
  • Haya ni yale yanayojijenga juu ya ardhi na kuhifadhi maji bila kunyauka kwa haraka. Kwenye TN 70, Jacob na Alvera Stern wanaelezea vizuri jinsi ya kuhusisha jamii hizi za wafugaji katika utengenezaji wa madimbwi haya.
  • Malambo madogo madogo ambayo hutengenezwa kwa kuweka kingo na kutandaza turubali la plastiki.

Mbinu: Kutumia mbinu za kisasa za uvunaji maji ya mvua ambazo zitapunguza mmonyoko wa udongo wakati huohuo kuhifadhi mvua nyingi aridhini pasipo kuacha yapite na kupotea kwa haraka. Mfumo huu waweza kuwa kwa kutumia njia zifuatazo;

  • Kuhifadhi maeneo ya miinuko/miteremko kwa kutengeneza matuta,kingo za mawe, mbinu za kilimo katika maeneo telezi – Sloping Agriculture Land technology (SALT) farming system  kwa kutumia gabions, demilunes  ama njia nyingine mbadala. 
  • Unaweza pia kupanda mbegu zako kwa kutumia mfumo wa “zai”. Zai ni mfumo wa shimo  ambayo mbegu hupandwa katika mashimo madogo yaliyochimbwa bila kutifua udongo katika vipimo vinavyoeleweka. Katika mfumo huu, kuta ndogo za mawe zinaweza kutengenezwa katika kingo za matuta ili kuwezesha maji mengi zaidi kutuama katika udongo.

Mbinu: Kutumia mbinu za kutakasa maji ya kunywa kwa matumizi ya binadamu. Mifano ya mbinu hizi ni; Aqua Clara. Aqua Clara ni chujio la maji kwa kutumia mchanga, changarawe na dumu na bomba la plastiki. Mfumo huu ni rahisi wa kuzalisha maji ya kunywa. Mbinu nyingine ni kutengeneza kibuyu chirizi.

Kilimo katika maeneo ya wafugaji

Mara nyingi ardhi ya wafugaji huifadhiwa kwa ajili ya malisho ya wanyama. Hata hivyo kwa sababu mbalimbali wafugaji wameona kuwa ni vema/muhimu kulima mazao mbadala ama kwa kuchanganya na ufugaji na sio ufugaji peke yake. Zifuatazo ni mbinu za kuwasaidia wafugaji katika kuzalisha mazao kwa utumiaji wa kuta ndogo za mawe na mashimo ya “Zai”:

Stone bunds used to enhance the water catchment capacity of zai pits

Makontua ya ‘zai’ ikitengenezwa na mawe 
Picha kwa ruhusa ya Chris Reij

Mbinu: Kuhamasisha mbinu za kilimo ambazo ni rafiki kwenye ardhi duni na kame ambazo zitaendana na mfumo wa maisha ya wafugaji. Miongoni mwa mbinu hizo ni kama;

  •  Mfumo wa kilimo hifadhi cha asili (farming God’s Way).  Mfumo huu utawawezesha wakulima kuhifadhi ardhi na kupunguza usumbufu wa ardhi/udongo na kuzidisha ufanisi wa virutubisho kwa kubadilishabadilisha mazao. Pia kwa kutumia mboji na mara chache mbolea kidogo za madukani kwenye maeneo ya kudumu kwa kilimo. Mbinu hii hupunguza matumizi ya maji shambani.
  • Mfumo wa mashimo ya “Zai” na SALT ambao umeelezwa katika kurasa zilizopita. Vipimo vya upana na urefu na nafasi kati ya mazao katika kitalu cha mashimo ya “Zai” vinaweza kutumika. Mfano:  upandaji miti yenye matumizi mbalimbali ambayo yaweza kuwa pia chakula cha mifugo. Maeneo ambayo mfumo wa SALT unatumika kuimarisha maeneo ya miinuko, mazao yanaweza kupandwa katikati mwa kingo na kingo. Japokua mbinu hii ya SALT ni muafaka kwenye maeneo yenye unyevu mwingi, lakini mimea hii na nafasi kati ya mazao yaweza kutumika kwa manufaa makubwa katika ardhi kame.

Mbinu: Kuhamasisha juu ya mazao muafaka kwa ajili ya ardhi kame. Zingatia mazao ya asili na matunda ya maeneo kame mfano; jujube (Ziziphus muaritiana), na mazao yenye uwezo wa kustahimili ukame kama mihogo, mbaazi, ulezi, mtama na viazi vitamu.

Mbinu: Kuonesha uwezekano wa kuzalisha mboga za majani. Mboga za majani hutoa virutubisho muhimu na hulimwa kwenye vitalu vodogovidogo karibu na mazingira wanaokuwemo watu ili kulinda kutoliwa na wanyama walio machungani. Njia zifuatazo zinaweza kutumika kuwezesha hili;

  • Upandaji wa mboga kwenye magunia ama mifuko ambayo huhitaji nafasi ndogo sana.
  • Hifadhi ya maji kwa njia ya “Hafiri” ambayo imeelezwa awali  kwa ajili ya umwagiliaji wa bustani  ndogondogo
  • Matuta ya vina virefu (deep dug beds) kulingana na ugumu wa eneo, hupunguza gharama ya pembejeo na kuboresha udongo.

Mbinu: Kufundisha njia changamano za kuzuia wadudu waharibifu na kufundisha viatilifu/ madawa mbadala ya ukuzaji wa mimea pamoja na ufundishaji wa teknolojia hifadhi ya mazao baada ya kuvuna.

Kutumia vyanzo vya nishati mbadala katika maeneo ya ukame:

Mbinu: Kutumia teknolojia ambayo ni muafaka ili kuongeza ufanisi wa vyanzo vya nishati vilivyopo. Mifano:

  • Tumia kinyesi/mbolea ya ngombe kutengeneza nishati ya gesi ambayo itatumika kwa kumulika na kupikia. Kwenye (ECHO TN 44, “Methane Digesters,” inaelezea sampuli ya utengenezaji  gesi ambayo inatumia maji kidogo na ni ya kudumu (Kwa masomo zaidi, angalia hapo chini).
  • Kutumia vitu kama mabaki ya vipande vidogovidogo nya mbao, sodasti/maranda ama taka za mimea ambazo ni za bei nafuu kama nishati mbadala ya kuni ama mkaa.
  • Kutumia majiko sanifu yenye matumizi madogo na nafuu ya nishati ya mafuta ili kupunguza kiwango cha kuni zinazotumika na moshi mwingi ambao ungezalishwa.(angalia EDN 85).

Mbinu: Matumizi ya nishati ya jua pale inapohitajika. Nishati ya jua inaweza kutumika kwa kumulikia na kuchaji betri/simu. Shirika lijulikanalo kama Global Cycle Solutions lina uwakala Tanzania ili kuwezesha kupatikana kwa mfumo rahisi na mahususi wa kielektroniki maeneo yya vijijini. Majiko ya sola yana kipingamizi kwani hayawezi kufanya kazi kukiwa na mawingu ama nyakati za usiku.

Kupunguza  upotevu wa chakula kwa kufuata njia sahihi za uhifadhi 

Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 6

Mbinu: Tengeneza vifaa vya kuhifadhia nafaka kwa gharama nafuu mfano vihenge vya udongo ama chuma. Uwezo wa kuhifadhi nafaka kwa muda mrefu utatoa mbadala kwa jamii ya wafugaji juu ya matumizi ya mazao ya chakula na biashara. Mfano; wangeweza kununua nafaka mara tu baada ya kuvunwa kwa gharama nafuu na kuuza kiasi ama chote wakati bei zimepanda.

Njia za kuhifadhi nafaka ni kama hizi zifuatazo:

  • Kihenge cha nyumbani cha kuhifadhia nafaka kilichoundwa na shirika liitwalo (Global Service Corps) kinaweza kuhifadhi magunia ya nafaka/mahindi 10 hadi 11 yenye uzito wa kilogramu mia moja kila moja. Kihenge hiki kinaweza kugharimu kiasi cha dola za kimarekani 57 (USD) kwa ajili ya vifaa vingine vya kujengea tofauti na mchanga pamoja na matofali. Tazama (EEAS 2013 DAY 3 presentantion, “Household Grain Storage”). 
  • Kihenge cha chuma ambacho kinaweza kutengenezwa na mafundi wa kawaida wa chuma, kinahitaji uwekezaji wa dola za kimarekani 30-100. Tazama EDN 112 na Postcosecha’s website). 

Mbinu: Matumizi ya teknolojia ya ukaushaji na kuhifadhi mboga za majani na matunda. Hii yaweza kupelekea kupata vyanzo vya mapato. Teknolojia ya ukaushaji na uhifadhi wa matunda na mbogamboga lazima uambatane na uelimishaji na utoaji taarifa juu ya jinsi ya kurejesha vyakula vilivyokaushwa kukubalika na namna ya kuviandaa na kupata chakula chenye ladha nzuri.

Njia za ukaushaji zaweza kuhusisha hizi zifuatazo:

Mbinu: Kuiwezesha jamii kujua njia za utengenezaji wa mazao ya maziwa na hifadhi ya nyama. Hii itaongeza njia za kujipatia kipato kwa kutumia rasilimali nyingi walizonazo wafugaji. Shirika la chakula duniani FAO limeeleza kwa undani juu ya haya. 

Kuhamasisha mabadiliko ya tamaduni katika jamii:

Zifuatazo ni mbinu ambazo zitawezesha jamii ya wafugaji kukabiliana na changamoto za kijamii.

Mbinu: Chanzo cha mabadiliko kutendeka katika mtazamo unaoshikiliwa na kukubalika na jamii ya kimataifa. Mtazamo wa kibiblia duniani umeweza kuelezea changamoto nyingi zinazozikumba jamii za wafugaji. Mfano; tazama muhadhara uliofanya na bwana Roger Sharland uliopewa kichwa cha habari kisemacho “A Biblical Basis to Motivate Rural Change” (2013 EEAS Day 3) Tazama (2013 EEAS Day 3) yaani “mtazamo wa kibiblia kuhamasisha mabadiliko vijijini”.

Mbinu: Hamasisha ujasiriamali wa kijamii. Hii itahusisha kuviwezesha viwanda vya asili vitakavyowezesha kuboresha maisha na wakati huohuo kuwawezesha wale wanaotaka kuleta mabadiliko chanya/mazuri katika kijamii.Best Practice Notes  - Assisting Pastoralists Image 7

Masoko ya mifugo yanaweza kuboreshwa kwa njia zifuatazo:

  • Kuhakikisha yanakuwepo mara kwa mara, kwa mfano, kila wiki kuwe na mnada miongoni mwa wanajamii husika.
  • Vyombo vya habari/ mfumo wa mawasiliano kuhakikisha taarifa zinatolewa kwa wakati muafaka juu ya bei, mzunguko wa wanyama na mlipuko wa magonjwa.

Pamoja na hayo, ni vema kutoa fursa za kibiashara kwa bidhaa za maziwa, utunzaji wa nyama pamoja na ukaushaji na utunzaji wa ngozi.

Mbinu: Kuundwa kwa benki za ushirika wa vijiji ili kuboresha jamii za vijijini na kuwezesha mfumo wa usawa katika kumiliki na kupata huduma za kifedha. Mbinu hii imeelezwa kwa undani kwenye (“For Further Reading” section).

Mbinu: Kutoa elimu juu ya aina aina mbalimbali za vyakula na virutubisho,  na kuongeza aina hizo mpya za lishe  kwenye mifumo yetu ya asili ya chakula. Katika kuyafanya hayo, ni lazima kutambua umuhimu na thamani ya vyakula vya asili. Utambuzi huo utasaidia jamii zilizo ndani ya makundi tofauti ya kifamilia.

Machapisho yaliorejewa (Kwa Kiingereza)

Catley A., J. Lind and I. Scoones. 2012. Pastoralism and Development in Africa, Dynamic Changes at the Margins. Rutledge

El Hadary, Y. 2012. Managing scarcity in the dryland of East Sudan; the role of pastoralist local knowledge in rangeland management. In Resources & Environment, http://article.sapub.org/10.5923.j.re.20120201.08.html

FAO and VSF Belgium. 2009. Pastoralist Field School P Guidelines for Facilitation. ECHO funded Regional Drought Preparedness Project, FAO of the United Nations, Rome, Italy and Vétérinaires Sans Frontières Belgium, Nairobi, Kenya

Global Service Corps. 2008. Hafir Water Catchment Project. http://www.globalservicecorps.org/site/hafirs/

Heffernan, C, F. Misturelli, and L. Nielsen. 2001. Restocking and Poverty Alleviation. University of Reading.

Hodgson, D. 1999. Pastoralism, Patriarchy and History: Changing Gender Relations among Maasai In Tanganyika. Journal of African History 40:41-65.

Hodgson, D. 2011. Being Maasai, Becoming Indigenous: postcolonial politics in a neoliberal world. Bloomington: Indiana University Press. 288 pages, ISBN-13: 978–0253223050. See review at: http://www.pastoralismjournal.com/content/2/1/27

Mace, R. 1988. A Model of Herd Composition that Maximises Household Viability and Its Potential Application in the Support of Pastoralists under Stress. Renewable Resources Assessment Group, Centre for Environmental Technology, Imperial College, 48 Prince’s Gardens, London SW7 1LU URL: www.odi.org.uk/sites/odi.org.uk/files/odi-assets/publications-opinion-files/5333.pdf

O’Neil, D. 2011. Patterns of Subsistence: Classifications of cultures based upon sources & techniques of acquiring food and other necessities: Pastoralism, Palomar College, CA http://anthro.palomar.edu/subsistence/sub_3.htm

Scoones, I. (ed). 1995. Living with uncertainty: New directions in pastoral development in Africa. London, Intermediate Tech Pubs.

UNHCR. 1998. Environmental Guidelines: Livestock in Refugee Situations. UNHCR, Geneva.

UNHCR. 2002. Conservation and Alternative Fuels. UNHCR, Geneva.Cooking Options in Refugee Situations: A Handbook of Experiences in Energy Conservation and Alternative Fuels: http://www.unhcr.org/406c368f2.html

Waters-Bayer, A. and W. Bayer. 1994. Planning with Pastoralists: PRA and more. Eschborn, GTZ

rejea nakala hii kama:

ECHO staff. 2019. Jarida la Mbinu Bora. ECHO Best Practices Note no.7.

Kwa Maelezo Zaidi (Kwa Kiingereza):

Kuhusu Ufugaji kwa Ujumla wake 

FAO. 1990. Community Forestry: Herders’ Decision-Making in Natural Resources Management in Arid and Semi-arid Africa. Community Forestry. Note No. 4. Rome. http://www.fao.org/docrep/t6260e/t6260e00.HTM

Arid Lands Information Network (ALIN) through Baobab magazine provides high impact options for interventions.

Tearfund “The impact of climate change on nomadic people.

LEGS. 2009. Livestock Emergency Guidelines and Standards. http://www.livestock-emergency.net/userfiles/file/legs.pdf

Bayer, W., and A. Waters-Bayer. Participatory monitoring and evaluation (PM&E) with pastoralists: a review of experiences and annotated bibliography. Eschborn: Deutsche Gesellschaft für Technische Zusammenarbeit (GTZ), 2002.

Kuboresha matumizi ya ardhi kwa jamii inayoishi katika maeneo ya wafugaji 

IEED. 2010. Participatory Land Use Planning as a Tool for Community Empowerment in Northern Tanzania. Ujamaa Community Resource Team. This features a highly participatory method that ensures whole village buy-in to the natural resource plans, increasing the likelihood that a community will adhere to the bylaws that are created. http://pubs.iied.org/pdfs/14608IIED.pdf

Mifumo muafaka yenye kulandana na ufugaji

Kuboresha utunzaji wa mifugo katika maeneo ya ukame 

Kutumia wasaidizi wa tiba ya mifugo vijijini 

Mbinu za kukidhi magonjwa ya kawaida ya mifugo 

Jinsi ya kuboresha matumizi ya idadi ya mifugo katika kikundi 

Restocking Pastoralists: A Manual of Best Practice summarizes the concept of restocking of livestock and contains links to decision-making materials.

Encouraging social entrepreneurship 

Kilimo katika maeneo yenye ukame 

Uzalishaji wa mazao 

  • Foundations for Farming
  • Zai pit system
    • TN 78
    • Kaboré D. and C. Reij. 2003. The Emergence and Spread of an Improved Traditional Soil and Water Conservation Practice in Burkina Faso Conference Paper No. 10: InWEnt, IFPRI, NEPAD, CTA conference, Pretoria. http://www.ifpri.org/ sites/default/files/pubs/events/conferences/2003/120103/papers/paper10.pdf

Mazao yanayokabiliana na ukame 

Mbinu za kutunza bustani katika maeneo yanye ukame

Matumizi ya vyanzo muafaka vya nishati

Nishati inayotokana na samadi ya mifugo (biogas) 

Majiku sanifu na upishi 

Nishati inayotokana na jua 

Global Cycle Solutions: Improving Village Life through Quality, Affordable Technology (with a subsidiary in Tanzania).

Kupunguza uharibifu wa chakula kwa kuhifadhi na kusindika kwa njia mbadala

Kuhamasisha mabadiliko ya tamaduni katika jamii