ceci Publication Issue n’existe pas dans votre langue, Voir dans: Kiswahili (sw),
Ou utilisez Google Traduction:  

Karanga ni mojawapo ya mazao yanayotoa mafuta. Katika Tanzania zao hili hustawi zaidi katika mikoa ya Kusini Mashariki, Dodoma na Morogoro. Pamoja na kutoa mafuta vile vile zao hutumika kwa njia nyingine mbali mbali, nazo ni pamoja na: Chakula cha wanyama / mifugo (Mashudu na majani), kurutubisha ardhi na chakula cha binadamu: kutafuna na kuunga kwenye mboga/chakula. Kwa ujumla zao hili hutumika na wakulima kama zao la biashara.