Este Publication Issue no existe en su idioma, Ver en: Kiswahili (sw),
O usar Google Translate:  

Kuna msemo usemao, mwenye juhudi na maarifa siku zote hufanikiwa katika jambo alifanyalo, bali mlegevu mafanikio hujitenga nae. Na anaeshinda siku zote tuzo ni haki yake. Hali hii imedhihirika pia kwa Mkulima Mbunifu. Tangu kuanzishwa jarida la Mkulima Mbunifu, tumekuwa tukishiriki kwa hali na mali katika shughuli za wakulima nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na kushiriki maonesho ya wakulima Nane Nane . Kwa mwaka huu, tumepiga hatua kiasi kikubwa kwa kuwa huduma yetu imeweza kutambulika zaidi miongoni mwa jamii ya wakulima na hata serikalini.