This Publication Issue does not exist in your language, View in: Kiswahili (sw),
Or use Google Translate:  
English (en) | Change Language

Kuku kama ilivyo kwa mifugo wengine, wanahitaji kuwa na banda, na kupatiwa matunzo sahihi. Kwa kufanya hivyo, utaweza kufahamu maendeleo ya mifugo yako na pia kujipatia faida kadhaa zinazotokana na ufugaji wenye tija. Moja ya faida hizo ni pamoja na mbolea, mayai, na idadi ya kuku wako kuongezeka. Ni hatari sana unapofuga kuku kiholela kwani hupotea ovyo kwa kuliwa na wanyama porini, wezi, kutagia porini sehemu ambayo huwezi kupata mayai kwa ajili ya chakula na hata kuuza. Pia, wanaweza kufa kutokana na magonjwa ya aina mbalimbali.