This Publication Issue does not exist in your language, View in: Kiswahili (sw),
Or use Google Translate:  
English (en) | Change Language

Katika jitihada za kutafuta namna ya kufikisha ujumbe kwa wakulima wengi zaidi kuhusiana na njia nzuri na sahihi zaidi za kilimo, MkM imeanzisha kipindi cha redio. Kipindi hiki kitasambaza kwa upana zaidi yale ambayo yamekuwa yakiandikwa katika jarida hili. Kipindi hiki cha redio kitakuwa kikiangazia mafanikio ya wakulima na wafugaji katika nyanja mbalimbali. Kipindi cha Mkulima Mbunifu kinarushwa na kusikika kupitia TBC Taifa na TBC Fm kila siku ya jumanne jioni, saa moja na robo hadi saa moja na nusu.